Saturday, May 14, 2005

MRADI WA KISWAHILI MOMBASA

Nawashukuru Nia na Haki walionipatia kiungo cha habari kuhusu mradi wa Kiswahili mjini Mombasa, Kenya. Nenda

WANATAALUMA WANAOBLOGU

Wanataaluma wengi sasa wanaanza kutumia blogu katika kazi zao na mambo yao binafsi. Bonyeza hapa.

SIKILIZA HOTUBA ZA MWALIMU NYERERE

Bonyeza hapa umsikilize Mwalimu Nyerere akihutubia.

Tuesday, May 10, 2005

JE UNAJUA?

BILA
CHINI
JUU
NDANI
NJE
ILA
HATA
BADO
HALAFU/KISHA
LABDA
MAANA/KWASABABU/SABABU
HIVI
VILE
VILEVILE
PIA
KATIKA

KUWA / KUWA NA

1. Mwaka jana ilikuwa mwanafunzi
2. Nina majirani watatu

MASWALI

MASWALI:
lini?
nini?
nani?
kwanini?
gani?
ngapi?
...je?

Tuesday, May 03, 2005

Naomba nionyeshe njia ya kwa fundi cherehani

Furaha: Naomba nionyeshe njia ya kwenda kwa fundi cherehani
Masanja: Fundi cherehani yupi?
Furaha: Unamkumbuka fundi cherehani aliyeshona gauni langu la krisimasi?
Masanja: Aah, panda basi la kwenda Kariakoo, shuka kituo cha Magomeni. Vuka barabara. Nenda upande wa pili. Utaona muuza madafu mkono wa kushoto, nenda moja kwa moja hadi utakapoona duka la madawa upande wa kulia. Chukua barabara ya mkono wa kushoto, nenda hadi utakapokuta njia panda. Ukifika hapo njia panda uliza mtu yeyote kwa fundi Mgonja.

Furaha anaandika maelezo yote kisha anamshukuru Masanja na wanaagana.

PANDE ZA DUNIA

Jua linachomoza kila alfajiri toka upande wa mashariki
Jua linazama alasiri upande wa magharibi
Antaktika iko ncha ya kaskazini ya dunia
Kuna baridi kali sana katika ncha ya kusini ya dunia

-ko, -po, -mo

Amani na Nabii wanaongea kwenye simu ya mkono.

Amani: Uko wapi?
Nabii: Nipo posta
Amani: Tumaini yuko wapi?
Nabii: Sijui. Labda yumo benki

** -ko: indefinite location
-po: definite location
-mo: refers to location inside

Monday, May 02, 2005

"KI" na "PO"

"KI":
1. Nikienda Tanzania nitapanda mlima Kilimanjaro
2. Kila nikila maharagwe ninajisikia kulala

"PO":
1. Nilipokwenda Tanzania nilipanda mlima Kilimanjaro
2. Kila nilipokula maharagwe nilijisikia kulala

AMBAYE, AMBAO, AMBACHO, AMBAYO....

M-WA
Umoja: Ambaye: mtoto niliyemtaja anakuja
Wingi: Ambao: watu niliowaona wanatoka Marekani

M-MI
Umoja: Ambao: mti ulioanguka ni mrefu sana
Wingi: Ambayo: miti iliyoanguka ni mirefu sana

KI-VI
Umoja: Ambacho: Kisu kilichonikata ni cheusi
Wingi: Ambavyo: Visu vilivyonikata ni vyeusi

KWENDA KWA HOSPITALI/ KWA DAKITARI

Nia: Shimakoo dakitari
Dakitari: Marahaba, habari
Nia: Nzuri kiasi, najisikia mgonjwa
Dakitari: unaumwa nini?
Nia: Ninaumwa kichwa na tumbo. Viungo mwilini vinauma na sina nguvu kabisa
Dakitari: Toka lini?
Nia: Toka juzi usiku
Dakitari: Umetumia dawa yoyote?
Nia: Ndio, nimekula panado kupunguza maumivu
Dakitari: Je unaweza kula chakula
Nia: Sina hamu ya kula kabisa. Nikila ninatapika
Dakitari: Je una....

Kabla Dakitari hajamaliza kuuliza Nia ananyanyuka.

Nia: Tafadhali naomba kwenda kujisaidia. Choo kiko wapi?
Dakitari: Choo cha wanawake kiko mlango wa pili, upande wa kushoto.

Nia anaondoka haraka haraka kwenda chooni. Anarudi baada ya dakika kumi.

Dakitari: Unapata haja vizuri?
Nia: Hapana, ninaendesha
Dakitari: Basi utakwenda maabara ukapime damu halafu utaniletea majibu.

Nia anakwenda kupima damu. Baada ya muda anarudi kwa Dakitari na majibu ya damu. Dakitari anasoma majibu kwa makini.

Dakitari: Naona una malaria. Nitakuandikia dawa ya malaria na nyingine ya kuendesha. Utatumia mara tatu kwa siku. Rudi hospitali siku ya jumanne asubuhi saa tatu. Ugua pole
Nia: Asante

KISWAHILI NI LUGHA YA KITAIFA NA KIMATAIFA

Soma insha hii ya kiingereza iliyoandikwa na Mukolozi wa Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam kuhusu Kiswahili kama lugha ya kitaifa na kimataifa. Hapa.