Naomba nionyeshe njia ya kwa fundi cherehani
Furaha: Naomba nionyeshe njia ya kwenda kwa fundi cherehani
Masanja: Fundi cherehani yupi?
Furaha: Unamkumbuka fundi cherehani aliyeshona gauni langu la krisimasi?
Masanja: Aah, panda basi la kwenda Kariakoo, shuka kituo cha Magomeni. Vuka barabara. Nenda upande wa pili. Utaona muuza madafu mkono wa kushoto, nenda moja kwa moja hadi utakapoona duka la madawa upande wa kulia. Chukua barabara ya mkono wa kushoto, nenda hadi utakapokuta njia panda. Ukifika hapo njia panda uliza mtu yeyote kwa fundi Mgonja.
Furaha anaandika maelezo yote kisha anamshukuru Masanja na wanaagana.

0 Comments:
Post a Comment
<< Home